Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao !!!

 

Nasaha za Dini  

"Mwenyezi Mungu akimtakia kheri Mja humfahamisha (humpa elimu) kwenye dini" Hadith Tukufu

NGUZO  ZA SWALA ...


6) KUITADILI BAADA YA RUKUU:

         Hii ndiyo nguzo ya sita katika mlolongo wa nguzo za swala. Na kuitadili maana yake ni kusimama na kulingana sawa baada ya kuinuka kutoka rukuu. Kwa hiyo tunaweza kabisa kusema kuwa kuitadili ni kisimamo sawa kinacho tenganisha baina ya rukuu na sijida.
Dalili ya Itidali: Itidali kama mojawapo ya nguzo za swala imetajwa katika riwaya iliyo pokelewa kutoka kwa Bi. Aisha-Allah amuwiye radhi-kwamba yeye aliielezea swala ya Mtume-Rehema na Amani zimshukie-akasema: “Alikuwa anapo kiinua kichwa chake kutoka rukuu, husujudu mpaka (kwanza) alingane sawa hali ya kusimama (aitadili)”.


Sharti za Itidali:
Ili Itidali iswihi, kumeshurutizwa mambo yafuatayo:
i. Kutokukusudia kwa kuitadili kutoka rukuu kitu kingine chochote zaidi ya ibada.
ii. Kutulizana katika Itidali kiasi cha kadiri ya kuleta Tasbihi moja.
iii. Asirefushe mno kisimamo cha Itidali kiasi cha kuzidi muda unaotumika katika usomaji wa Suratil-Faatihah. Hii ni kwa sababu Itidali ni miongoni mwa nguzo fupi, kwa hivyo basi hakujuzu kuitwawilisha (kuirefusha).

7) KUSUJUDU MARA MBILI KATIKA SWALA:
Nguzo ya saba ya swala ni kusujudu. Na maana ya sijida ni kugusa paji la uso la mswaliji mahala anapo sujudu.
Dalili ya sijida: Sijida kama nguzo ya swala ni agizo na amri ya Allah itokanayo na kauli yake tukufu: “ENYI MLIO AMINI! RUKUUNI NA SUJUDUNI NA MUABUDUNI MOLA WENU NA FANYENI MEMA, ILI MPATE KUFAULU”.2
Na kauli yake Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-alipo mwambia yule mtu aliye kosea katika swala yake: “...Kisha sujudu mpaka utulizane hali ya kusujudu. Halafu inuka utulizane hali ya kukaa, halafu sujudu (tena) mpaka utulizane hali ya kusujudu...”.
Sharti za sijida:
Ili sijida iswihi kisheria, kumeshurutizwa kuchunga mambo yafuatayo:
a) Paji la uso liwe wazi wakati wa kugusana na ardhi.
b) Kusujudu kuwe ni kwa viungo saba alivyo vitaja Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-kupitia kauli yake: “Nimeamrishwa kusujudu kwa (kutumia) mifupa (viungo) saba; Juu ya paji la uso – na akaashiria kwa mkono wake pua yake – na mikono na miguu na ncha za (vidole vya) miguu”.3
Tanbihi: Si wajibu kuacha wazi chochote katika viungo saba hivi vilivyo tajwa ila paji la uso tu.
c) Sehemu yake ya chini (kiuno) iinuke zaidi kuliko ile ya juu (mabega) kiasi kimkinikacho. Kufanya hivyo ni kufuata kitendo cha Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie.
d) Hasisujudu juu ya nguo iliyo ambatana naye inayo tukutika kwa mtukutiko wake, mithili ya kilemba au kashida yake.
e) Hasikusudie kitu kingine chochote zaidi ya sijida, mithili ya kuporomoka kwa ajili ya hofu.
f) Kukandamiza kidogo paji lake katika ardhi kwa sura ambayo kama ingekuwepo hapo anapo sujudu pamba au kitu mithili ya pamba, ingebonyea na athari ya sijida kudhihiri hapo.
g) Kutulizana katika sijida kwa kadiri ya kuleta Tasbihi moja.
Na ukamilifu wa sijida ni mswaliji kuleta Takbira ya kuporomokea sijida na kuweka ardhini magoti yake yakifuatiwa na mikono. Halafu paji na kumalizia na pua yake na aiweke mikono yake welekeya (mkabala) wa mabega yake na avitandike vidole vyake kwa kuvikusanya vikiwa vimeelekezwa Qiblah. Na aliepushe tumbo lake kugusana na mapaja yake, na dhiraa zake zisigusane na ardhi wala mbavu zake. Na aseme mara tatu: SUB-HAANA RABBIYAL-A’ALAA. Imepokelewa kutokana na hadithi ya Abu Hurayra-Allah amuwiye radhi-katika kuielezea swala ya Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie: “...Kisha husema: ALLAAHU AKBAR, wakati aporomokapo hali ya kusujudu...”.4
Na imepokelewa kutoka kwa Abdillah Ibn Maalik Ibn Buhaynah-Allah amuwiye radhi-kwamba Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-alikuwa anaposwali, huweka mwanya baina ya mikono yake mpaka unaonekana weupe wa kwapa zake”.5
Imepokewa kutoka kwa Al-Baraai-Allah amuwiye radhi-amesema: Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-amesema: “Unapo sujudu, basi weka vitanga vyako (ardhini) na vinyanyue viko (mirfaq) vya mikono yako”.6
Na imepokewa katika kutaja wasifu wa swala ya Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie: “...na anapo sujudu, husema katika sijida yake: SUB-HAANA RABBIYAL-A’ALAA, mara tatu...”.7
Tanbihi: Mwanamke huhitilafiana na mwanaume katika baadhi ya vipengele tulivyo vitaja. Yeye ataukusanya pamoja mwili wake wakati wa kusujudu. Imepokelewa kwamba Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-aliwapitia wanawake wawili hali ya kuwa wanaswali, akawaambia: “Mnapo sujudu (kuelekea ardhini), basi zikusanyeni baadhi ya nyama, kwani mwanamke siyo kama mwanaume katika hilo”.8 

8) KITAKO BAINA YA SIJIDA MBILI:
Kitako hiki baina ya sijida mbili ni wajibu kiwepo katika kila rakaa.
Dalili ya kitako hiki:  Kitako hiki kilicho baina ya sijida mbili; ile ya kwanza na ya pili, kimetajwa katika kauli yake Bwana Mtume-Rehema na Amani zimshukie-iliyo pita: “...Halafu inuka utulizane hali ya kukaa...” [Rejea dalili za sijida]
Sharti za kitako baina ya sijida mbili: Kumeshurutizwa katika kuswihi kwa kitako hiki, kuchunga mambo yafuatayo:
Akusudie ibada kwa kitako chake hicho na siyo kingine chochote, mithili ya kukaa kwa sababu ya hofu.
Asikitwawilishe (asikirefushe) sana kitako hicho kiasi cha kuzidi muda wa uchache wa Tashahudi.
Kutulizana kiasi cha kuleta Tasbihi moja.

9.                 KIKAO CHA MWISHO.

Hapa kinachokusudiiwa ni kile kitako kinachokuwa katika rakaa ya   mwisho ya  swala, kinachofandamiwa na salamu.

Ni suna iliyothibiti  kukaa mkao wa “ Tawarruki”  katika kikao hiki cha  mwisho . Huu ni  mkao ambao mtu hukalia tako la kushoto  na sehemu  ya tako la kulia , akaunyoosha  mguu wa kulia kama unavyokuuwa katika si  jida na kuupitisha ule wa kushoto chini yake.

Imekuja kaatika  riwaya ya Abuu  humayd : “ ……………..hata ilipokuwa sijida ambayo ndani yake   ndimo imo salamu ( sijida ya mwisho )  huutoa  mguu wake wa  kushoto na akakaa mkao wa tawarruki kwa kukalia tako lake la kushoto” Abuu Daawound

 

10.           TASHAHUDI YA MWISHO { KATIKA KIKAO  CHA MWISHO}

Ni wajibu kwa mwenye  kuswali akae  baada  ya sijda ya  mwisho ya swala yake asome “Tashahudi”  imepokelewa katika riwaya ya Ibn  Masoud Allah amuwiye radhi – amesema : Tulikuwa tukisema kabla ya kufaradhishwa juu yetu Tashahudi  

ASSALAAM ALALLAH KABLA IBADIHI, ASSALAAM ALAA JIBRILL, ASSALAAM ALA MIIKAIL, ASSALAAM ALA FULAN

Mtume   - Rehema na amani zimshukie  alipomalizaa kuswali alituelekkea , akatuambia “ Hakika  Allah ndiye AS – SALAAM , basi anapokaa mmoja wenu  katika   swala { Kwa  ajili ya Tashahudi } basi  na aseme  

ATTAHIYYAAT LILLAH WASSALAWATU WATTAYYIBAATU, ASSALAAM ALAYKA AYYUHA NNABII WARAHMATULLAH WABARAKATUH, ASSALAAM ALAYNA WA-ALAIBADILLAHI SSALIHINA

Kwani  nyinyi mtakapoisema {salamu  hii}  humpata {humfikia} kila mja mwema mbinguni na ardhini. Bukhaari na  Muslim.

Hili  ni mojawapo ya matamko  sahihi ya   Tashahudi ambayo  yaliyonukuliwa kutoka kwa Bwana  Mtume. Tashahudi yeyote iliyothibiti kutoka kwa Mtume mtu  akiisoma itamjuzia.

Sharti za Tashahudi.

Msomaji  wa Tashahudi analazimika kuchunga yafuatayo:

  1. Ajisikizishe  yeye  mwenyewe matamko ya Tashahudi  iwapo hana tatizo la kusikia.

  2. Kukifululiza kisomo cha tashahudi, yaani asiweke mwanya mkubwa baina ya ibara za Tashahudi . pia asitie kati dhikri nyingine , akifanya hivyo yaani akinyamaza kinyamao kirefu au  akilia kati dhikhri  nyingine , Tashhahudi yake  itakuwaa imebatilika na itamuwajibikia kuianza upya.  

  3. Aisome katika hali ya kukaa isipokuwa katika mazingira ya dharura tu ndio anaruhusiwa kuisoma  katika hali  yoyote imkinikiayo.

  4. Aisome kwa lugha ya Kiarabu . Akishindwa atasoma tafsiri yake kwa Lugha  yake, Lakini bado atakuwa na wajibu wakujifunza mpaka aweze kuisoma kiarabu kama alivyofanya Mtume wa Allah- Rehema na Amani zimfikie.  

  5. Achunge  matokeo ya herufi , shada na hukumu zote za usomaji . akifanya kosa lolote litakalopelekea  kuharibika  kwa maana,  halitamaanisha zaidi ya  kubahatilika Tashahudi yake  hiyo . Kwa  hivyo basi itamlazimu kuirejea upya .

  6. Ayatungamanishhe maneno ya Tashahudi  kwa mtungo wake kama yalivyopokelewa kutoka kwa Mtume wa Allah – Rehema na Amani  zimshukie .

 

 




Forum | Guestbook | Tuandikie |