|
9: Takbiyrah za
kugura
Tumeshajua
katika masomo yaliyotangulia kwamba “Takbiyrah ya kuhirimia swala” ni nguzo
ambayo swala haisihi bila ya kuileta. Takbiyrah hii ndio inayoashria mwanzo
wa swala na kwamba tayari umo ndani ya swala. Sasa unapokuwa ndani ya swala
ndipo inapokuja suna ya “Takbiyrah za maguro”. Hizi ni kusema mwenye kuswali
(ALLAAU AKBAR) wakati
-
Anapokwenda rukuu
-
Anapokwenda sijda, na
-
Anapoinuka kutoka sijda aidha kuja katika kitako baina
ya sijida mbili au kuja kuanza rakaa nyingine.
ANGALIA
si suna kuleta “Takbiyrah ya kugura” wakati wa kuinuka kutoka rukuu kuja
itidali bali suna ni kusema: SAMIA’ -LLAHU LIMAN HAMIDAH. Haya yote ndiyo
maelekezo tunayoyaopata kutokana na hadithi aliyoipokea Abuuu Hurayrah Allah
amuwiye radhi amesema Alikuwa Mtume wa Allah Rehema na Amani zimshukie
anaposimama kwenye swala hukabiri (huleta Takbiyrah) wakati anaposimama
(Qiyaamu) na hukabiri anaporukuu, kisha husema: SAMIA’ -LLAHU LIMAN HAMIDAH
wakati anapounyoosha mgongo wake kutoka rukuu, halafu ndipo husema akiwa
amesimama wima: RABBANAA WALAKAL-HAMDU. Kisha hukabiri wakati anapoporomokea
sijida, halafu hukabiri (tena) wakati anapoinua kichwa chake (kutoka sijida
ya kwanza. Halafu hukabiri (tena) wakti anaposuiju (sijida ya pili) kisha
hukarbiri (tena) wakati anapokiinua kichwa chake (kuja kuanza rakaa
nyingine). Halafu hufanya hivi hivi katika swala yote mpaka anapoimaliza na
kukabiri (pia) wakati anapoinuka kutoka katika rakaa mbili (za mwanzo) baada
ya kjitako (cha tashahudi ya kwanza).” Bukhaary na Muslim.
10.
Tasbihi za rukuu na sijida:
Ni
suna kwa mwanamume ajiachie wakati wa kurukuu na kusujudu yaani ngoko za
mikono yake zisigusane na mbava zake. Ama mwanamke, suna kwake ni
kujikusanya, yaani ngoko zake zigusane na mbavu zake bila ya kuachia nafasi.
Kisha ni suna aseme ilhali ametulizna katika rukuu: SUB-HAANA RABBIYAL-A’DHIM
Mara tatu, na asema katika sijida SUB-HAANA RABBIYAL-A’ALAA Mara tatu. Hivi
ndivyo ilivyopokelewa kutoka kwa Hudhayfah Ibn Alyamaan Allah amuwiye radhi
amesema “Niliswali pamoja na Mtume wa Allah Rehema na Amani zimshukie
alipoenda rukuu akawa akisema: SUB-HAANA RABBIYAL-A’DHIM Kisha alisujudu na
akasema SUB-HAANA RABBIYAL-A’ALAA.” Muslim na Ibn Hibbaan.
11. Kuweka mikono (vitanga)
mwanzoni mwa mapaja katika vitako vya tashahudi.
Namna
ya uwekaji ni mtu kukitandika/kukikunjua kitanga cha kushoto ilhali
amevikusanya pamoja vidole bila ya kuvitawanya kiasi ambacho ncha za vidole
zitakuwa zimeelekeana na mwanzo wa goti. Akikunje kitanga cha kulia isipokuwa
kidole cha shahada, hiki atakikunjua kwa kukiinamisha mwanzoni mwa tashahudi
mpaka atakapofikia kusema ILLA-LLAH ndipo atakiinua kuashiria kwamba Allah ni
mmoja. Na ni suna aendelee kukiinua bila ya kukitikisatikisa mpaka mwisho wa
swala, yaani kutoa salamu. Imepokelewa kutoka kwa Ibn Umar Allah awawiye
radhi amesema katika kuuelezea ukaaji wa mtume Rehema na Amani zimshukie
Alikuwa anapokaa ndani ya swala huweka kitanga chake cha kulia juu ya paja
lake la kulia na akakunja vidole vyake vyote na akaashiria kwa kidole chake
ambacho kinachokifuatia kidole gumba (cha shahada) Na huliweka kitanga chake
cha kushoto juu ya paja lake la kushoto.” Muslim.
12.
Mkao wa “Tawaruki” katika kikazi ha mwisho na mkao wa “Iftiraashi katika
vikazi vingine vyote.
“Tawaruki”
huu ni aina ya mkao ambao mwenye kuswali hulikalia tako lake la kushoto na
akaunyoosha mguu wake wa kulia na kuutolea ule wa kushoto chini yake (ule wa
kulia) Na “Iftiraahsi” ni mkao ambapo mtu hukikalia kisigino cha mguu wake wa
kushoto na kuunyoosha ule wa kulia kwa kuziweka chini ncha za vidole. Imepokelewa
kutokana na hadithi ya Abuu Humayd Allah amuwiye radhi amesema: Mtume wa
Allah Rehema na Amani zimshukie kuliko nyie (na akasema katika sehemu ya
hadithi hiyo): Na anapokaa katika zile rakaa mbili (za mwanzo) huukalia mguu
wake wa kushoto na kuukunjua ule wa kulia (Tawaruki). Na anapokaa katika ule
mkao wa mwisho huutanguliza mguu wake wa kushoto (yaani chini ya mguu wake wa
kulia aliounyoosha) na akaunyoosha ule mwingine na akayakalia makalio
(matako) yake.” Bukhaariy
13.
Kumswalia Mtume kwa kutumia
“Swalaatu Ibraahimiyyah” kasha kumba dua baada ya Tashahudi ya mwisho.
Tayari
umekwishafahamikiwa katika masomo yaliyotangulia kwamba kumswalia Mtume ni
nguzo miongoni mwa nguzo za swlaa ambazo swala haisihi kama hazikuletwa:
Nguzo hii hutekelezwa kwa kumswalia mtume kwa tamko lo lote lile linalobeba
maana ya kumswalia. Lakini suna kumswalia kwa kuleta “Swalaatu
Ibraahimiyyah,” hii ni kusema
ALLAHUMMA
SWALLI ALAA MUHAMMAD WA ‘ALAA AALI MUHAMMAD KAMAA SWALLAYTA ALAA IBRAHIM WA
‘ALAA AALI IBRAHIM, WABARIK ALAA MUHAMMAD WA ‘ALAA AALI MUHAMMAD KAMAA
BAARAKTA ‘ALAA IBRAHIM WA ‘ALAA AALI IBRAHIM INNAKA HAMIIDUN MAJIID
Bukhaariy
Akimaliza
kumswalia mtume kwa tamko hili au kwa matamko mengine ni suna amuombe Mola
wake amkinge/amuepushe na adhabu ya kaburi, na adhabu ya moto. Au aombe dua
yo yote aitakayo kwa shariti asitwawilishe (asiirefushe) dua hiyo zaidi ya
muda ule anaoutumia kusoma tashahudi na kumswalia mtume.
Imepokelewa
kutoka kwa Abuu Hurayrah Alah amuwiye radhi amesema: Amesema Mjume wa Allah
Rehema na Amani zimshukie:- “ Atakapomaliza mmoja wenu (kusoma) Tashahudi ya
mwisho, basi na ajilinde kwa Allah dhidi ya mambo manne: adhabu ya moto wa
Jahanamu, adhabu ya kaburi, na fitina ya uhai na kifo na shari ya masihi
Dajali.” Muslim
14. Salamu ya pili
Tumeeleza
katika darasa zilizopita kwamba salamu ya kwanza katika swala, ambayo hii
ndio huashiria kumalizika kwa swala ni nguzo. Hii ni ile inayoambatana na
kugeuka upande wa kulia wakati wa kuitoa. Pamoja na kwama salamu hii ya
kwanza inamaanisha kumalizika kwa swala lakini ni suna kuongezea kutoa salamu
ya pili huku ukigeukia upande wa kushoto. Hivi ndivyo alivyopokea Ibn Masoud
Allah amuwiye radhi kwamba Mtume wa Allah Rehema na amani zimshukie alikuwa
akitoa salamu kuliani na kushotoni kwake mpaka unaonekana weupe wa shavu lake
ASSALAAM ‘ALEYKUM WARAHMATULLAH, ASSALAAM ‘ALEYKUM WARAHMATULLAH
Abuu
Daawoud
Miongoni
mwa dua alizokuwa akiomba Bwana mtume ni ile iliyopokelewa na Imamu Aliy
Allah amuwiye radhi kwamba Mtume wa Allah Rehema na Amani zimshukie “Alikuwa
akisema baina ya Tashahudi na salamu.
ALLAHUMMA-GHFIR
LII MAA QADDAMTU WAMAA AKHHARTU WAMAA ASRARTU WAMAA A’LANTU WAMAA ASRAFTU
WAMAA ANTA A’LAMU BIHI MINNIY ANTALMUQADDIM WA ANTALMUAKHHIR LAA ILAHA ILLA
ANTA
Muslim
Hizi
zote kwa ujumla ndizo suna zinazoitwa “hay-aata”, suna hizi kama
tulivyotangulia kueleza mwenye kuswali akiacha ye yote miongoni mwake si suna
kwake kuiunga kwa kuleta “sijidat sahau”.
|