|
SIJIDA
YA KUSAHAU (SIJIDATIS–SAH–U).
AINISHO/MAANA
YA KUSAHAU:
Neno
“Kusahau” lina maana mbili kama ifuatavyo:-
I.
KUSAHAU KILUGHA:
Katika lugha ya kawaida kusahau kunamaanisha
kupoteza kumbukumbu za kitu/jambo au kughafilika
na jambo. Bila ya kujali kuwa upotezaji huu wa
kumbukumbu ni wa muda tu au ni wa milele.
II.
KUSAHAU KISHERIA (KIFIQ-HI):
Muradi na
mapendeleo ya neno “kusahau”
katika somo letu
hili ni yale makosa
(kunguwao)
anayoyafanya mwenye kuswali ndani ya
swala yake.
Bila ya kuangalia amefanya makosa
hayo kwa bahati mbaya
(kwa kusahau) au kwa
makusudi mazima.
FALSAFA/HEKIMA
YA SIJIDA YA KUSAHAU:
Sheria
ya Kiislamu
imeyazingatia maumbile ya mwanadamu na
kumuona kuwa
ni kiumbe dhaifu
anayesahau
na kukumbuka kwa kuyazingatia maumbile
haya ya mwanadamu ndipo
sheria
ikamuwekea kiumbe huyu
“Sijida ya
kusahau” katika swala yake ili:-
Amfukuzilie
mbali shetani anayemtia
katika
wasiwasi
huu wa kusahu.
Ayazibe
makosa ambayo kwa namna moja au nyingine anaweza
kuyatenda ndani ya
swala
yake.
iii)HUKUMU
YA SIJIDA
YA KUSAHAU:
Sijida hii ya kusahau inaweza kuwa
ama ni wajibu au
ni suna.
Wakati
gani sijida ya kusahau inakuwa ni WAJIBU?
Sijida ya kusahau inakuwa wajibu wakati
ambapo mwenye
kuswali anapokuwa
maamuma nyuma ya Imamu
wake. Imamu wake huyu atakaposahau na kusahu kwake huku kukampelekea kusujudu
kwa sababu ya kusahau huko. Akasujudu
sijida ya kusahau katika hali hii
kutamuwajibikia maamuma
aliye nyuma ya Imamu huyu kumfuata Imamu
wake katika kusujudu huko hata
kama yeye
(maamuma) hakusahau. Angalia
maamuma huyu atapomkhalifu Imamu wake
asimfuate katika huko kusujudu swala
yake itabatilika na kutamuwajibikia
kuirejea tena (kuiswali upya.
Wakati
gani sijida ya kusahau inakuwa SUNA ?
Sijida
ya kusahau itakuwa ni suna
wakati ambapo mwenye kuswali atapoacha
cho chote ambacho si katika jumla ya
nguzo za swala
kama kuacha kuleta Qunuut katika
swala
ya Sub-hi au swala ya Witri ya Ramadhani.
DALILI/USHAHIDI
WA SIJIDA YA KUSAHAU:
Sijida
ya kusahau
imethibiti katika Suna ya
Mtume. Imepokelewa kutoka kwa Abuu
Hurayrah–Allah amuwiye radhi– amesema:
“Mtume wa Allah-Rehema
na Amani zimshukie: Alituswalisha swala
ya Adhuhuri au ya Alasiri, akatoa salamu.
Dhul-yadaini akamwambia: Swala
ewe Mtume wa Allah, je imepunguzwa
(idadi ya rakaa zake)? Mtume akauliza:
“Ni kweli ayasemayo (Dhul-yadaini)?
(Maswahaba) wakasema: Naam, (Mtume) akaswali
rakaa mbili nyingine, kisha akasujudu sijida mbili”. Bukhaariy
Tutazitaja
dalili nyingine wakati tutakapotaja sababu za
kusujudu sijida ya kusahau.
MGAWANYO
WA MATENDO YANAYOWEZA KUACHWA NA MWENYE KUSWALI
NDANI YA SWALA YAKE:
Matendo
ya swala
ambayo mwenye
kuswali anaweza kuyaacha ndani ya swala
yake ama kwa makusudi au kwa kusahau,
yanagawika katika mafungu matatu. Ima
mwenye kuswali atakuwa ameacha tendo
linalloitwa:-
FARDHI
na pia huitwa NGUZO, au
2.
SUNAH na sunah ikusudiwayo hapa ni ile
inayoitwa
“Ba’adh”.
SUNAH
isiyo “Ba’adh”, yaani suna iitwayo
“Haiah”. Hii ni kama vile Takbira za
maguroguro (kuhama kutoka Qiyaamu kwenda
rukuu, kutoka Itidali kwenda
sijida na
kadhalika) na kunyanyua/kuinua mikono
wakati wa kuleta Takbira ya kuhirimia
swala.
HUKUMU
ZINAZOANDAMIA MATENDO HAYA:
FARDHI:
Tendo la fardhi/nguzo lililoachwa
kwa makusudi HUBATILISHA swala
na lile lililoachwa kwa makusudi
halikaliwi badali, yaani haliungwi na sijida ya
kusahau.
2.
SUNAH BA’ADH: Tendo la Sunah
mithili ya Tashahudi
ya mwanzo, mkao wake, Qunuut. Mwenye
kuswali akisahau kuleta cho chote miongoni mwa
matendo haya, atapaswa
kusujudu sijida ya kusahau.
SUNA
HAIAH: Tendo linaloingia chini ya
sunah hii ni mithili ya Tasbihi za
rukuu,
sijida na kadhalika.
Mwenye
kuswali
hawajibikiwi kusujudu kwa kusahau bila ya
kuangalia kuwa aliacha makusudi au kwa
kusahau.
SABABU
ZA SIJIDA
YA KUSAHAU:
Mambo
yafuatayo ndio yatakayo mpelekea mwenye kuswali
kuleta sijida ya
kusahau:
-
Mwenye
kuswali kuacha
mojawapo
miongoni
mwa suna za swala zinazoitwa
“Ab-aadh”, mithili ya Tashahudi ya
mwanzo na Qunuut
(kwa ufafanuzi wa kina juu ya suna
hizi, rejea SURA YA PILI, SOMO LA KWANZA,
SWALA {x} Suna za swala). Imepokewa kutoka
kwa Abdullah Ibn Buhaynah-Allah amuwiye
radhi–kwamba yeye amesema: Mtume wa Allah–Rehema na Amani zimshukie-alituswalisha
rakaa mbili za
swala fulani. Na katika upokezi
mwingine: “Aliinuka
kutoka katika
rakaa mbili za
swala ya Adhuhuri, kisha akasimama na
wala hakukaa (Tashahudi
ya mwanzo), watu (maamuma)
nao wakainuka pamoja nae. Alipomaliza
swala yake
(kwa kuswali rakaa mbili za mwisho),
(wakati) tukiingojea salamu yake,
akakabiri (akasema Allahu
Akbar) kabla ya kutoa salamu.
Akasujudu
sijida mbili na il-hali amekaa,
kisha (ndio) akatoa salamu.
Bukhaariy &
Muslim.
Imepokelewa
kutoka kwa Al-Mughiyrah Ibn
Shu’ubah–Allah amuwiye
radhi–amesema: Amesema Mtume wa Allah–Rehema
na Amani zimshukie:
“Atapoinuka mmoja wenu kutoka (katika) rakaa mbili
(za mwanzo) na
akawa hajatimia hali ya
kusimama , basi na akae (kwa
ajili ya Tashahudi ya mwanzo. Na
atapotimia
hali ya kusimama, basi na asikae
(aendelee na
swala yake)
na atasujudu sijida mbili
za kusahau”.
Ibn Maajah,
Abuu Daawoud & wengineo.
-
Mtu
kuwa na shaka ya
idadi ya rakaa alizoziswali. Katika
hali hii, mwenye shaka anatakiwa aishike
idadi ya chini na atimize rakaa
zilizobakia.
Kisha
atasujudu
sijida ya kusahau
kwa ajili ya kuunga imkani ya kwamba
yeye amezidisha
kitu katika swala yake. Lau mtu
atakuwa
na
shaka je,
ameswali
Adhuhuri rakaa
tatu au nne? Shaka hii ikamtokea
akiwa bado
ndani ya
swala, basi atachukulia kuwa
ameswali rakaa tatu na aongeze rakaa
moja nyingine ili zitimie rakaa nne zitakiwazo. Halafu
tena
akimaliza asujudu sijida mbili za
kusahau kutokana na imkani ya kuwa kaswali rakaa tano na
hivyo kuwa amezidisha kitu
katika
swala yake.
Imepokelewa
kutoka kwa Abuu Said–Allah
amuwiye radhi–amesema: Amesema Mtume wa
Allah–Rehema na Amani zimshukie:
“Atapotia shaka mmoja wenu
ndani ya swala yake,
na asijue ameswali rakaa ngapi, tatu au
nne? Basi (cha
kufanya) ni kuitupa
shaka hiyo na ajengee
alicho na yakini nacho. Kisha asujudu sijida mbili kabla
ya kutoa salamu. Akiwa
ameswali rakaa tano, (kusujudu huko)
kutaifanya
swala
yake
kuwa jozi
(ya
rakaa
mbili za
mwanzo
na mbili za
mwisho).
Na
akiwa ameswali kutimiza rakaa nne, zitakuwa
(sijida
mbili) hizo zimemdhalilisha na
kumghadhibisha shetani”. Muslim.
Ama
lau mtu alitia shaka
nje ya swala (baada
ya kutoka ndani
ya swala) kwa yakini shaka yake hii
haitaathiri usahihi na ukamilifu wa swala
yake. Ila kama shaka hiyo itakuwa ni
katika nia na
Takbira ya kuhirimia swala,
shaka hii itamlazimisha
kuirudia (kuiswali tena) swala yake.
TANBIHI:
Kusahau
kwa maamuma wakati wa kumfuata Imamu wake, kama
vile kusahau Tashahudi ya
mwanzo. Kusahau kwake huku kutachukuliwa
na Imamu wake na wala haitamlazimu kusujudu
sijida mbili za kusahu baada ya
salamu ya Imamu wake. Dalili ya
haya ni kauli yake Bwana
Mtume–Rehema na Amani zimshukie:
“Imamu ni mdhamini
(wa
maamuma)”. Ibn Hibbaan
|