Makala
Mwanzo
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao

 

  MASWALI NA MAJIBU-Biashara na Riba  


Biashara na Riba-Sehemu ya Kwanza                              
 
  1. naomba kuuliza swali kuhusu kuchukua deni bank ambalo kama kawaida lina riba je ina juzu.mimi nina nafasi yangu kibiashara na wala sichukui deni bank kwa shida ila katika kuendeleza biashara zangu tu.

  2. (1)Mimi naishi ulaya na ni mwanafunzi jee, naweza kuchukua mkopo toka serikalini ambapo masharti ni kwamba mkopo huu natakiwa ni urudishe pindi nipatapo kazi baada ya kumaliza masomo? na sharti la mkopo ni kwamba riba inaanza kuhesabiwa tu pindi mtu anapopata kazi na kabla ya kupata kazi kama utarudisha huo mkopo basi hauna riba.Na mkopo wote unaweza kusamehewa kama utaihama nchi kabisa kabisa. Jee, sheria inaniruhusu kuchukua huo mkopo?kama ninaweza kufanya hayo niliyo yaeleza?
     
    (2)Muislamu anaruhusiwa kumuoa ahlulkitaab? na jee, ndio hawa wakiristo?

  3. suali ni hili - kuwa mimi nafanya kazi bank na nimeshajenga nyumba kwa njia ya bank - na mengi tu na pia sipendi kuchukuwa live ila ramadhani na nakuwa naenda umra jee sasa umra yangu inasihi na hii kazi ni ya haramu ? sasa na nyumba nimeikodisha napokea kodi jee sasa hizi pesa niharamu? na pia nna mama ni mgojwa zanzibar kila mwezi anahitaji dawa na mimi ndio nnapeleka pesa jee yaani sipati dhawabu?  naomba msisaidie kwa suali hili. Wallah bitofiq.

  4. Swali langu ni juu ya Hijja au Umra,moja ya sharti la kuswihi kwa Hijja kipato halali.Mimi nafanya kazi hivyo kipato changu ni halali na ninataka kwenda UMRA.Benki kawaida kunakuwa na riba.Je UMRA yangu itaswihi? naomba ufafanuzi hapo nifanyeje?

  5. swali langu mimi nimtu kutoka sultanate of Oman swali kuna mama mmoja kutoka emarat UAE anasema anatoa sadaka kwa kuwa yeye anaumwa kansa saa yoyo yote ile ana weza kufa sasa yeye ana toa sadaka lakini kwanza lazima watu kutoka Oman lazima alipe riali 100 baada ya miezi miwili alielipa  riali 100 ana pata riali 500  yani mtu ana weza kutoa kiwango chochote kile anacho weza yani kili mia ana pata 500 na ukitoa 200 una pata 1000 na anasema yeye hii ni jammiya khaiyria sasa nina taka kujua hii ni RIBA au sio RIBA   naomba mnijibu haraka sana iweze kanavyo na mnifaha mishe hatari ya riba mbele ya mwenyezi mungu 

  6. INAFAA IKIWA MSHAHARA WANGU UNATIWA BANK NA KWA VILE PESA NYINGI MIMI SITOWI ZOTE HUWENDA KUTOWA ZILE NNAZOZIHITAJIA, NA SIJAFUNGUA ACCOUNT YENYE FAIDA, KUACHA KULE KWA AJILI YA HIFADHI PESA NYINGI KUZIWEKA NYUMBANI. MASHEKHE WANATAKHLIFIYANA WENGINE WANATUAMBIA HAIFAI KUWEKA PESA HATA BANK.

  7. mimi ninakaa nyumba ya kukodi maisha yangu, mwenye nyumba anaitaka nyumba yake, sasa mimi ninataka kuchukuwa mkopo na uwe mkopo wa riba wa kunua nyumba baada ya kulipa kodi hizo pesa zende katika mkopo wa nyumba baada ya miaka 20 itakuwa nyumba yangu.nimilipa nyumba ya kukodi miaka 10. nikiendelea kukodi miaka yote nikikuwa siwezi kufanya kazi nitakaa wapi. mwenye nyumba atanitoa.

  8. Mimi nimekopa pesa kutoka benki ili nifanyie mambo yangu ya kimaendeleo na benki wamekubali lakini kwa sharti kuwa itanibidi nilipe asilimia 19 ya kiasi nilichokopa wakati wa kurudisha hilo deni. Je hiyo ndiyo riba iliyokatazwa? kama ni riba je mabenki yatawezaje kujiendesha na kutoa huduma ya kutunza pesa za watu kwa usalama, kwani wapo wafanyakazi, majumba na ulinzi? vyote hivyo vinahitaji pesa.

  9. nina mdogo wangu wa kike kaolewa kiasi miaka miwili nyuma yeye mashaalla kashika dini lakini alipoposwa na mtoto wa shangazi yetu ambaye anafanya kazi bank alikubali na akamuowa,baada ya mwaka yule mumewe akaacha kazi ya bank sasa anafanya kazi kwenye company tu,jee mahari yake alopokeya ni haramuna ndoa yake ni haramu au laa, nini anatakiwa afanye ikiwa ni haramu? Shukran

  10. Naomba kujua iwapo uislam unaruhusu watu kuwekeana vitu rahani(kuweka poni).ahsante

 

JIBU

 

                                                                          


| Tuandikie |