- KUNA
MTU ANAUMWA NA MARADHI YA PUMU. AKAMUHADISIA
MTU YALE MARADHI YAKE. YULE MTU AKAMWAMBIA
NTAKUPA DAWA UNAWEZA UKAFANYA, AKAMUULIZA
DAWA GANI AKAMWAMBIA KUWA SIKU ILE ILE WATU
WANAO CHINJA HUKO MACCA SIKU YA SKUKUU (MUNA)
SIKU ILEILE NA WEWE ULIKO CHINJA MNYAMA KAMA
(MBUZI AU NGO'MBE,NGAMIA AU KONDOO) KISHA
KUNYWA PALEPALE ILE DAMU YA YULE MNYAMA PUMU
ITAONDOKA, SASA ANAWASIWASI KUFANYA
HIVYO WATU WENGINE WANAMWAMBIA HARAMU KUNYWA
DAMU YA MNYAMA, SASA NAOMBA MNISAIDIYE
HILI SUALA.
2.
MIMI
NIMEFANYA IBADA YANGU YOTE YA HIJA IKABAKI SIKU
ILE YA KWENDA KUFANYA TAWAF YA KUAGA KUKAWA NA
ZAHMA KUBWA SANA TUKASEMA TUTAKWENDA SIKU YA
PILI NIKAPATA DAMU YANGU YA HEDHI IKAWA SIJENDA
KUAGA TENA NIMERUDI KWENYE NCHI YANGU.
KWA
HILI JAMBO LILILO NITOKEA INATAKIWA KUFANYA KITU
CHOCHOTE.
- Jee
mtu anaweza kwenda kuhiji kama ana deni? au
lazima alipe madeni yake kabla ya kwenda? Na
kama hana hizo pesa kwa kipindi kile
anaruhusiwa kwenda kuhiji?
- Je
ni sahihi kwamba mtu akienda Makka kuhiji
akirudi anakuwa amefutiwa dhambi zake zote
za nyuma? Je siku ya hesabu atahesabiwa
kuanzia aliporudi kutoka Makka au tangu
abalehe.
- Moja
ya shuruti za hijja au umra ni kipato halali.
Swali je mimi kama sifanyi kazi lakini mume
wangu ndio amenigharimia safari ya kwenda
huko,je hiyo inakubalika?
- katika
kuzunguka kaaba unatakiwa kuzunguka
mizunguko saba.
Swali je unaweza ukaamua kufanya zaidi ya
hiyo saba? au haitakiwi kuzidisha
- Swali
langu ni juu ya dua unapokunywa maji ya
zamzam, je ni lazima unukuu kutoka katika
quran? au unaweza kutumia maneno yako
mwenyewe? inasemekana ni vizuri unapokunywa
maji ya zamzam usome dua nyingi,naomba
ufafanuzi hapo yaani dua (ombi) zaidi la
moja mfano unaomba kuponywa maradhi au
katika ombi lako hilo moja ulitilie mkazo
kwa dua nyingi?
- je
unapokoga kabla ya kuanza ibada ya umra
kunakuwa na manuizo katika kukoga huko?
Kama lipo nuizo naomba nuizo hilo (dua).
Swali jingine,je naweza kuwaombea wanangu
na wazazi wangu? na ni wakati gani mzuri kwa
dua kama hiyo?baaba ya kumaliza ibada ya
umra au katika sala za fardhi(swala tano).
- swali langu ni juu ya ibada ya umra. pale unapokuwa katika kituo cha
ihram ni sunna kukoga,je hayo maji unayokoga
ni maji ya kawaida(bombani) au ni maji
ya zamzam?
Swali la pili nini hikma ya kukoga
kabla ya kuanza ibada hiyo ya umra?
JIBU
|