|
|
| |
MASWALI
NA MAJIBU-Ndoa na Talaka |
| |
|
| Ndoa
na Talaka -Sehemu
ya Sita |
|
|
|
|
|
- Habari
za kazi pole na majukumu mimi nina swali
kidogo,nauliza mvulana amemchumbia msichana
ili amuoe
bahati mbaya baada ya kukubaliwa posa yake
wakazini
mvulana na huyo msichana na akapata mimba
sasa yule
mvulana kuona hali imekuwa hivyo akaamua
kwenda kwao
ili aoe mambo yaishe, sasa ndoa yao
inakubaliwa na
Mwenyezi Mungu ama la naomba ufafanuzi mzuri
inshallah
ni hilo tu sina la zaidi ahsante.
- Mimi
ni mwanamke, Nina haki ya kudai talaka iwapo
sitendewi haki na mume wangu? Kama ninayo,
nitumie hatua zipi? Kama Sina Nifanye nini?
- swali
langu ni hili pindi mwanamke akiacha sala
imeamriwa kuwa aambiwe mara tatu na mumewe
kama hakusikia ahamwe kitandani na ni hukumu
gani juu ya mwanamume? pia huwenda nikawa
nimekosea kufafanua swali naomba mnisaidie
- 1.nataka
kujua ushahidi wa mwanaume kuzini.ili
ushahidi huo umtie hatiani.
2.je katika hukumu ya kiislamu kukata rufaa
kunakujaje?ikiwa hukumu ya kwanza tayari ni
hakika katika sharia kiislamu
- kuwa
akiwa mumeo haswali analewa jee - kwa sisi
wanawake tufanye nini kukaa nae mume huyu ni
halali or haramu ? kama ni haramu pia kudai
talaka nimesikia kuwa unaingia motoni moja
kwa moja. kwani talaka ni halali lakini
Allah anaichukia. sasa naomba nasiha. na
mimi katika wanawake wanoimani kwani sasa ni
mwaka wa 18 hali ndio hii. nasubir naamin
faraja iko karibu lakin ni taaban lakin bado
nasubiri kama kuna dua naomba mnisaidie
ndugu zangu. nakungoja jawabu yenu.
- Napenda
kuuliza masuala ya haki za ndoa.
(a) Inapasa mume na mke kuishi mbalimbali
kwa muda wa zaidi ya miaka miwili bila ya
sababu yoyote?
(b) Mume anaeitelekeza familia yake bila ya
kutoa matumizi ya chakula na malazi kwa muda
wa mwaka mmoja,jee,mwanamke atahisabiwa kama
bado ni mke au kaachika?
(c) Mwanamume asiekua na nguvu za kiume
inampasa kuoa?
- naomba
kuuliza suala langu hili, kuhusu kujitia
manukato, mume amehawil sana kuzungumza na
mkewe kuhusu akitoka nje asijitie mkewe
manukato ya aina yoyote udi au mafuta, na
mwanamke jawabu hawezi kutoka bila kujitia
manukato na mume amechoka kumkataza, sasa
analo ogopea asije akavunja ndoa juu yao,
tunaomba suluhisho la watu hawa wawili baina
ya mume na mke. ni nini?
- ikwa
mtu anamtiii mumewe na mumewe anakuwa
anamdhania maovu , kama anazini akirudi
nyumbani kutazama nyumba nzima kama mkewe
kaeka mtu , au akirudi nyumbani anamcheki
nyweli kama zimekoshwa , hee hebu nisaidieni
mtu kama huyo mwanamke afanye nini na
anakuwa taabani na mambo anayofanya mumewe
- Nimeolewa
na mume ambaye alisilimu miaka 12
iliyopita,kabla hajanioa.
Aliachana na mkewe wa Kikristo kabla hajawa
Muislam,ambaye wakati anamuoa alimkuta na
watoto 2 wa Kikristo na aliishi naye kwa
miaka 3 tu na kuachana.Sasa,baada ya miaka
12,ameanza kuwasiliana tena na wale watoto
wake wa kufikia,Kiasi cha kuwapeleka cinema
wakati wa mwezi mtukufu wa Ramadhan.Mimi
niliona siyo sawa Kiislamu,na tulienda kwa
Imamu,lakini Imamu kasema si Haramu yeye
kujihusisha na wale watoto.
Je,hii ni kweli? mbona tumeelezwa kwenye
sura ya Al I'mran aya ya 100,kuwa
tusijihusishe nao na sura nyinginezo pia?
- Baada ya kufanya ndoa na mwanamke asiye mwislamu, kubahatika kupata
watoto na mwishowe kufikia mfarakano
kuachana kisheria kwa nchi tuishiyo. Na
kwamba yote tangu wakati ndoa hata
kuachana kwetu kumefanyika nje ya dini yaani
hakuna sheikh wala kadhi aliyehusika, bali
kufanyika kama vile katika ofisi. Je inanibidi nifanye nini kuhusu watoto baada ya
kuachana na mama mtu?
JIBU
Rudi
Nyuma
|
|
|
|
|
|
| |
|
|
| Tuandikie |
| |
|