|
|
|
|
|
| Zaka-Sehemu
ya Kwanza |
|
|
|
|
|
- Shekh
Nakuomba Saana msaada wako kwa kutufafanulia
aya hizi zifuatazo nazo
ni: Qurani 9:60, 9:103, na 2:280. katika
eneo hili la hapa keko ninaposali kumetokea
kutoelewa baada ya kuchanganywa
na madai ya kwamba:
1. ZAKA na SADAKA ni kitu kimoja -katika
jinsi-ya-kutolewa na watumiaji-pia.
2. Na kwamba ikiwa mtu akikusudia kukupa/kukuzawadia
hata chungwa-moja-tu na akatamka
neno 'SADAKA' basi inakuwa ni kharamu kula
ikiwa wewe sio miongoni mwa Fakiri au
Masikini n.k kwa mujibu wa Qrn 9:60. Eti kwa
ufafanuzi unavyodai.
** Na hali hii ilianzia wakati wa mwezi
mtukufu wa ramadhani kidogo kidogo
wakati huo kulikuwa na muislamu aliyeamua
kugawa futali kwa baadhi ya
misikiti na wetu ukawa ni mmoja wapo, Sasa
ikawa imamu wetu anapotangazia
kuwa "Jamanie kuna SADAKA ya futali
katika msikiti wetu kwahiyo waislamu
tuhudhurieni katika kupata chochote kilicho
andaliwa na muislamu mwenzetu
Inshaallah."
Basi mzozo ulianza polepole kwamba ukitamka
neno SADAKA 'kama atakula
muislamu ambaye anaouwezo wa kupata futali
basi ni KHARAMU-KULA maadamu limetamkwa tu
neno SADAKA. Yafaa itamkwe IK-RAM!!!. Au
ukitaka kumpa muislamu
mwenzio kitu, Basi useme hivi: "Aisee
nakukirimu kitu kadha.." Na wala
usiseme nakupa SADAKA yangu kitu Kadha..!!!
2. Na maneno haya SADAKA na ZAKA
yanafafanuliwa kama ifutavyo:
*Sadaka na Zaka nikitu kimoja tu wala havina
utofauti wowote -hata katika
kutolewa kwake.
*Sadaka ni kusema ukweli, na Zaka ni
Kutakasika. kwa mujibu wa Qrn. Kwahiyo
mtu anapotangaza mali yake ki-ukweli kabisa
hiyo huitwa SADAKA, na mtu
anapolipa zaka ya halali ndiyo kutakasika!!!.
Kwahiyo imedaiwa kwamba Zaka na Sadaka ni
kitu kimoja tu na wapewaji ni kwa mujibu wa
Aya hizo hapo juu hasa Qrn 9:60.
<>Na ama baadhi yetu tumeamua
kulifuatilia swala hili lakini tunagonga
ukuta
kutokana na udhaifu wa vitabu na hasa elimu
ndogo ya uchambuzi qurani kwa
kina.
--------------------------
KWAHIYO SHEKH: NDIYO MAANA MIMI PAPOJA NA
WAISLAMU WENZANGU TUMEAMUA
TUKUULIZIE WEWE NA UTUSAIDIE JUU YA MZOZO
HUU KUPITIA MASWALI YETU HAPO
CHINI:
1 Nini Maana, Na matumizi ya maneno haya:
SADAKA na ZAKA?
2 ZAKA inatolewaje? na sadaka?
3 Je, Shekh mimi nikiamua kukupa wewe tunda
kama mf. wa embe kisha nikatamka kwamba:
"karibu sadaka ya tunda". itakuwa
wewe kuchuwa ni kharamu maadamu unao uwezo
wa kulinunua?
-----
4. Mwisho kabisa Nakuomba unisaidie, Website
ambayo inayochambua KILA AYA kwa HADITHI,
ASS'BABU N-NUZL, MAF-HUMU YAKE, mfano kama
tafsiri ya IBUN KATHIIR. Na mengineyo kama
Hayo.
Ikiwa ya Lugha ya i.Kiswahili, ii.Kiingereza,
au ii.Kiarabu.
tumejaribu kuitembele website ya www.al-islam.com:
katika hadithi, qurani
nk. na pia www.islamzine.com
lakini hatukupata msaada wowote. Juu ya mada
hii.
Tunatarajia jibu lolote kutoka kwako (Hata
kwa ufupi tu), ilituweze
kujikwamua na mashaka haya Inshaallah. Na
Hasa tusaidie sana Maombi yetu ya
nambri 4. hapo juu.
- 1.
jee zakaa ni halali kutoa kwa asikua
muislamu?
2. vile vile fungu lipi ni kubwa zaidi kwa
unapotoa zakaa baina ya muislamu na asiekua
muislamu?
- Ukiwa
unafanya kazi na unapokea mshahara mfano
laki moja kwa mwezi je kuna haja za
kuzitolea zaka.
- Swali
langu linahusu Zakaa, Je! Nalazimika
kuzitolea Zakaa kwa pesa nnazozidai? na
sijui ntalipwa lini?
- INAJUZU
KUZIGAWA PESA ZA ZAKA YA DHAHABU KATIKA
SEHEMU YA NYUMBA 5,LAKINI UKANUNUWA CHAKULA
KAWAPELEKEA KATIKA KILA NYUMBA, ILI
KIWAFAE KWENYE HUU MWEZI MTUKUFU WA
RAMADHANI. AU LAZIMA ZITOLEWE PESA.
- INAWEZEKANA
IKIWA KATIKA KILA MWEZI WA RAMADHANI
HUWA NIKITOWA ZAKAA YA DHAHABU.
KATIKA MWAKA HUU TUMEPATA MSIBA WA NDUGUYETU
AMEWACHA WATOTO WA MAYATIMA WADOGO HAWAJABALEKH.WATOTO
WA YATIMA WANAISHI KATIKA NCHI YA EST
AFRICA. INAFAA KUTOWA PESA KUWANUNULIA
NGUO NA KUWAPELEKEA NGUO ZIWAFAE KWA SKUKUU.
INAJUZU BADALA YA KUTOWA HIZI PESA KUWAPA
WATU HAPA NCHI ZA GULF,
TAFADHALI NISAIDIYENI HILI SUALA LANGU.
- naomba
kuuliza suala langu ni kuhusu almasi, almasi
inatolewa zaka.na ikiwa inatolewa zaka
inaaanza kutolewa kwa kiwango gani?
- Swali
langu ni kuhusu Zakaa. Je nina lazima kutoa
Zakaa kwa pesa nilizokwishazitolea mwaka
uliopita?.
Kwa mfano Mwaka ulipita nilikua na Shs
10,000/ nikazitolea Zakaa, Na mwaka huu zile
pesa zimeongezeka kua Shs 15,000/ Swali ni
kua itabidi nizitolee zile zilizoongezeka tu
yaani Shs 5,000/ au Zote kwa jumla? Naomba
jibu.
- Ninauliza
ikiwa mimi ni mwanafunzi na nilikuwa
nikitenga pesa kadha ninazopewa shule. Je
ninao ulazima wa kuzitolea ZAKKA? kwa nini?
- Mtoto mchanga aliyezaliwa mwezi wa Ramadhani inafaa kumtolea Zakaat Al
Fitr?.
JIBU
|
|
|
|
|
|
| |
|
|
| Tuandikie |
| |
|