Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao !!!

 

SIRA YA MTUME (SAW)  

"BILA SHAKA MNAO MFANO MWEMA KWA MTUME WA MWENYEZI MUNGU…"Al-qur-an (33:21)

SOMO LA NNE
MSIMAMO WA QURAN KWA WALIOACHA KWENDA VITANI BILA UDHURU HALALI

 Faida

 

       I.       Msimamo wa Qur-ani Tukufu ulikuwa ni mkali mno kwa wale walio acha kwenda katika medani ya vita bila ya kuwa na udhuru halali:

         Kwa ajili hiyo basi, Qur-ani Tukufu ilishikilia msimamo mkali kabisa kwa wale ambao waliacha kwenda vitani bila ya kuwa na udhuru – zingatiwa. Ikawalaumu na kuwaumbua, ikawafedhehesha na kuwasifia uduni, upomoshi wa hima na upuuzi. Na kwamba wao hawayachangamkii ila manufaa/maslahi ya dunia na malengo yenye kuondoka. Ama amali tukufu na mambo adhimu, wao si wadau wala watafutaji wake: “NA LAU INGELIKUWA IPO FAIDA YA PAPO KWA PAPO, NA SAFARI YENYEWE NI FUPI, WANGELI KUFUATA. LAKINI WAMEONA NI MBALI NA KUNA MASHAKA. NAO WATAAPA KWA ALLAH: TUNGELI WEZA BILA YA SHAKA TUNGELI TOKA PAMOJA NANYI. WANAZIANGAMIZA NAFSI ZAO. NA ALLAH ANAJUA KUWA HAKIKA HAO NI WAONGO......NA MONGONI MWAO WAPO WANAO KUSENGENYA KATIKA KUGAWA SADAKA. WANAPO PEWA WAO HURIDHIKA NA WAKITO PEWA HUKASIRIKA”. [9:42-58]

Qur-ani ikazidi kuwaaibisha kwa uoga, ushindwa na upite na kwamba wao si miongoni mwa wenye ukwasi wakati wa shida/matatizo. Na wala si miongoni mwa wenye msaada wakati wa khatari na wanaipenda raha/starehe iliyo rahisi kuliko sulubu iliyo tukufu. Na wanaifadhilisha salama iliyo dhalili/duni juu ya khatari iliyo tukufu: “NA WANAAPA KWA ALLAH KWAMBA WAO NI KATIKA NYINYI, WALA WAO SI KATIKA NYINYI. LAKINI NI WATU WANAO OGOPA. LAU KAMA WANGELI PATA PA KUKIMBILIA AU MAPANGO AU MAHALA PA KUINGIA, BASI WANGELI FYATUKA MBIO KUELEKEA HUKO.........NA INAPO TEREMSHWA SURA ISEMAYO: MUAMININI ALLAH NA PIGANENI JIHADI PAMOJA NA MTUME WAKE, WALE WENYE NGUVU MIONGONI MWAO HUKUTAKA RUHUSA NA HUSEMA: TUACHE TUWE PAMOJA NA WANAO KAA NYUMA! WAMERIDHIA KUWA PAMOJA NA WABAKIAO NYUMA, NA NYOYO ZAO ZIKAPIGWA MUHURI; KWA HIVYO HAWAFAHAMU” [9:56-87]

Qura-ni ikaibainishia jamaa (kikundi cha waislamu safi walio kuwa pamoja na Mtume wa Allah kwa dhati ya nia) kwamba hao (wabakiao nyuma) ni fisadi na uchafu katika jamaa. Na kwamba kukaa kwao wasende vitani, kulikuwa ni bora zaidi kwa jamaa kuliko kutoka kwao. Na kwamba salama ya jamaa ni kusafishwa safu zao  kutokana na watu hao, kwa sababu wao hawayaamini malengo ya jamaa na wala hawashirikiani nao kihisia. Na kwa sababu wao katika jamaa ni vitenda – kazi bomozi na si vitenda – kazi vijenzi: “NA INGELI KUWA KWELI WALITAKA KUTOKA BILA YA SHAKA WANGELI JIANDALIA MAANDALIO, LAKINI ALLAH KACHUKIA KUTOKA KWAO, NA KWA HIVYO AKAWAZUIA NA IKASEMWA: KAENI PAMOJA NA WANAO KAA! LAU WANGELI TOKA NANYI WASINGELI KUZIDISHIENI ILA MACHAFUKO, NA WANGE TANGA TANGA KATI YENU KUKUTILIENI FITNA. NA MIONGONI MWENU WAPO WANAO WASIKILIZA. NA ALLAH ANAWAJUA MADHAALIMU. TANGU ZAMANI WALITAKA KUKUTILIENI FITNA, NA WAKAKUPINDULIA MAMBO JUU CHINI, MPAKA IKAJA HAKI NA IKADHIHIRIKA AMRI YA ALLAH, NA WAO WAMECHUKIA. NA MIONGONI MWAO WAPO WANAO SEMA: NIRUHUSU WALA USINITIE KATIKA FITNA. KWA YAKINI WAO HIVYO WAMEKWISHA TUMBUKIA KATIKA FITNA. NA HAKIKA JAHANNAMU IMEWAZUNGUKA. UKIKUPATA WEMA UNAWACHUKIZA, NA UKIKUSIBU MSIBA WAO HUSEMA: SISI TULIANGALIA MAMBO YETU VIZURI TANGU KWANZA. NA HUGEUKA KWENDA ZAO NA WAMEFURAHI........WATAKUAPIENI KWA ALLAH MTAKAPO RUDI KWAO ILI MUWAACHILIE MBALI. BASI WAACHILIENI MBALI, HAKIKA HAO NI NAJSI, NA MAKAZI YAO NI JAHANNAMU, KUWA NI MALIPO KWA WALIYO KUWA WAKIYACHUMA. WANAKUAPIENI ILI MUWE RADHI NAO. BASI HATA MKIWA RADHI NAO NYIYE, ALLAH HAWI RADHI NA WATU WAPOTOFU” [9:46-96]

Hivi ndivyo ulivyo kuwa msimamo wa Qur-ani kuwaelekea wanafiki na watafuta manufaa miongoni mwa wabakiao nyuma wakaepukana na safu za jamaa. Iliwadunisha na kuwatweza kutokana na hali yao na ikawaweka pale walipo jiweka wao wenyewe; yaani pamoja na walio bakia nyuma miongoni mwa wanawake, watoto, washindwa (wagonjwa) na wanyonge. Na ikalifichua suala lao kwa jamaa na kuihadharisha dhidi ya khadaa zao na ikawaamrisha kujitenga nao. Na zama walipo kuja kwa Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-wakitaka udhuru, alikupa nyongo kuwalaumu. Na badala yake akawakubalia dhahiri ya udhuru wao na kuiacha siri (undani) yao kwa Allah.

Ama wale ambao walijitegemeza kwenye ucheleweshi na wakalazwa na ulegevu kwa sababu ya uvivu na kupondokea ubwete. Na kujitia vivulini katika wakati wa joto kali, haikuwasukuma kutenda hivyo shaka yo yote na wala haukuwapelekea kutenda hivyo unafiki wala vitimbi. Hawa, toba yao ilikubaliwa na Allah na akampa idhini Mtume wake kuwasamehe. Na akamuamrisha kuwatakabalia baadhi ya mali zao wanazo zitoa kwa ajili ya Allah, ili kuzitwahirisha nafsi zao. Na kwa ajili ya kutangaza kukubaliwa kwao katika safu za jamaa na kuituliza khofu yao kwa kuwaombea kwake. Na azitulize nyoyo zao kwa kuwaswalia na kwa kurejea msamaha na maghfira ya Allah kwao: “NA WENGINE WALIKIRI DHAMBI ZAO, WAKACHANGANYA VITENDO VYEMA NA VINGINE VIOVU, ASAA ALLAH AKAPOKEA TOBA ZAO. HAKIKA ALLAH NI MWENYE KUSAMEHE MWENYE KUREHEMU. CHUKUA SADAKA KATIKA MALI ZAO, UWASAFISHE NA UWATAKASE KWAZO, NA UWAOMBEE REHEMA. HAKIKA MAOMBI YAKO NI UTULIVU KWAO. NA ALLAH NI MWENYE KUSIKIA MWENYE KUJUA. JE! HAWAJUI YA KWAMBA ALLAH ANAPOKEA TOBA YA WAJA WAKE, NA ANAZIKUBALI SADAKA, NA KWAMBA ALLAH NI MWINGI WA KUPOKEA TOBA NA MWENYE KUREHEMU? NA SEMA: TENDENI VITENDO, NA ALLAH NA MTUME WAKE NA WAUMINI WATAVIONA VITENDO VYENU. NA MTARUDISHWA KWA MWENYE KUJUA SIRI NA DHAHIRI; NAYE ATAKUAMBIENI MLIYO KUWA MKIYATENDA: [9:102-105]

 

    II.       Toba ya Ka’ab Ibn Maalik na wenzake wawili:

         Na walikuwemo miongoni mwa walio bakia nyuma wasende vitani, watu watatu walio mwambia ukweli Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie. Hawa hawakutunga uwongo na wala hawakupindua maneno, wakaliweka suala lao mikononi mwa Allah awahukumu atakavyo. Watatu hawa ni; Hilaal Ibn Umayyah, Muraarah Ibn Rabee na Ka’ab Ibn Maalik. Na katika kisa cha Ka’ab Ibn Maalik – kama kilivyo pokewa na wapokezi wengi – kuna sura/picha iliyo kwenda kina ya nafsi yenye hisia za mbali, iliyo muumini katika ukweli wake. Na katika ufumbulizi wake, dhiki yake na uhemevu wake, na katika uwokovu wake na furaha yake, na katika usafi wa niya yake na toba yake. Na taswira nyingine ya jamii ya Kiislamu katika kupanda kwa mwamko wake na utukufu wa kudiriki kwake mambo na hisia zake kali katika kuelewa dhambi ya mwenye dhambi na toba ya mtubiaji. Ka’ab Ibn Maalik anasema: “...ilikuwa katika khabari yangu pale nilipo bakia nyuma na Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-nisende pamoja nae katika vita vya Tabuuk. Kwamba katu mimi sikuwa mwenye nguvu mno na mwepesi sana, kuliko pale nilipo bakia nyuma nisende pamoja naye katika vita hivyo. Wallah, sikupata kukusanya kwangu kabla ya vita hivyo vipando viwili hata nikavikusanya katika vita vile. Na wala Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-hakukusudia vita ila alificha muelekeo wake. Mpaka vikawa vita vile, Mtume wa Allah akapigana katika joto kali na akaikabili safari ya mbali na maadui wengi. Basi Mtume akawawekea wazi suala lao (ya kuwa wanaelekea wapi) ili wajiandae vya kutosha na safari hiyo, akawaeleza muelekeo wake alio ukusudia. Na waislamu walio kuwa pamoja na Mtume wa Allah ni wengi, basi hapana mtu ye yote aliye taka kughibu (kutoweka) ila alidhania kwamba hili litafichikana maadam wahyi haujateremka kutoka kwa Allah aliye tukukia.

Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-akapigana vita vile wakati wa upendezi wa matunda na vivuli vya miti. Mtume wa Allah na waislamu walio kuwa pamoja naye wakajiandaa, nami nikadamka kujiandaa pamoja nao, basi hurudi na ilhali sijakidhi cho chote, basi hapo hujisemea: Mimi ni muweza juu ya hilo nikitaka. Basi hali hiyo haikuacha kunitambalia mpaka watu wakamaliza maandalizi yao na kuwa tayari kuondoka. Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie pamoja na waislamu wakaanza kuondoka nami nikiwa sijakidhi cho chote katika matayarisho yangu. Nikajiambia: Nitajiandaa baada yake kwa siku moja au mbili, halafu nitawakuta njiani. Basi baada ya kuondoka, mimi nikadamka kujiandaa, sikukidhi cho chote, nikadamka tena halafu nikarudi bila ya kufanya cho chote. Basi nikaendelea hivyo mpaka wakaenda zao haraka na ikanipita fursa ya kuvidiriki vita vile. Nikakusudia kusafiri ili niwadiriki njiani – eeh laiti mimi ningeli fanya hivyo – lakini hilo halikukadiriwa kwangu. Basi ikawa ninapo watokea watu baada ya kuondoka kwa Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie. Ikanihuzunisha kwamba mimi sioni kwangu kigezo ila mtu atuhumiwaye kwa unafiki au mtu miongoni mwa walio pewa udhuru katika wanyonge. Na Mtume wa Allah hakunikumbuka mpaka alipo fika Tabuuk, akauliza ilhali akiwa amekaa na maswahaba Tabuuk: “Amefanya nini Ka’ab Ibn Maalik?”, akajibu mtu katika Baniy Salamah: “Ewe Mtume wa Allah! Kumemshughulisha kujiona kukamzuia kutoka”. Muaadh Ibn Jabal akasema: “Maneno mabaya yaliyoje uliyo yasema! Wallah, ewe Mtume wa Allah! Hatujui kuhusiana naye ila kheri tupu”. Mtume wa Allah akanyamza kimya, hakusema lo lote.

Ka’ab anaendelea kusema: “Zama ilipo nifikia khabari kwamba Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-anarudi kutoka Tabuuk, ukanipata mtapo tapo wa moyo. Nikaanza kukumbuka uwongo nikijisemea: Ni kipi kitakacho niokoa na ghadhabu yake kesho? Nikamtaka msaada juu ya hilo kila mwenye busara katika watu wangu. Palipo semwa kwamba Mtume wa Allah amekaribia kuingia Madinah, batili yote ikaniondokea na nikatambua kwamba mimi sitaokoka kwake kwa kusema uwongo, nikatinda kumwambia ukweli. Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-akafika na ilikuwa ni ada yake anapo toka safari hufikia msikitini kwanza akaswali rakaa mbili. Kisha ndipo hukaa kwa ajili ya kuwasikiliza watu, alipo keti wakamjia walio bakia nyuma wasende vitani, wakitoa udhuru kwake na wakimuapia. Na walikuwa kiasi cha watu themanini na kitu, Mtume wa Allah akazikubali dhahiri zao na akawafanyia baia na kuwaombea maghfira. Na akazitegemeza na kuziacha siri zao kwa Allah, mpaka nikaja mimi mbele yake....

 



 | Tuandikie |