Makala
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao !!!

 

SIRA YA MTUME (SAW)  

"BILA SHAKA MNAO MFANO MWEMA KWA MTUME WA MWENYEZI MUNGU…"Al-qur-an (33:21)

HALI YA KIJAMII NA TABIA ZA WAARABU

 

Tumeeleza huko nyuma kwamba yalipatikana makabila mengi ya kiarabu kutokana na kizazi cha Nabii Ismail. Kila kabila liliundwa kutokana na kaya/familia kadhaaa zilizojiunga pamoja. Kila kabila liliongozwa na kiongozi aliyekuwa mtu mzima anayeheshimika, kukubalika na kutiiwa na wote. Ukabila ulikuwa ndio sera ya kila kabila, na kila kabila lilikuwa tayari kuilinda sera yake hiyo ya ukabila dhidi ya uadui wa wote ule kutoka makabila mengine kwa gharama yoyote ile. Msimamo huu na sera hii ya ukabila ilisababisha mizozo, ugomvi na mapigano ya mara kwa mara baina ya makabila haya. Kugombea vyanzo vya maji, machungo na kujifakharisha kwa nasabu pia vilichochea kwa kiasi kikubwa mizozo na mapigano.

Kama ambavyo watu hutofautiana katika vyeo/hadhi, kazi na hali za kimaisha, Waarabu pia waligawanyika katika matabaka yafuatayo:-

  1. Mabwana/Viongozi: hawa ndio waliokuwa na mamlaka juu ya wengine na hatamu za uongozi zilikuwa chini yao.
  2. Makuhani: hawa walikuwa ndio viongozi wa kidini wakiyatawalia mambo yote yanayohusu dini ikiwa ni pamoja na ibada, sherehe za kidini na mengineyo.
  3. Wafanyabiashara: hawa walijishughulisha na usambaji na uuzaji wa bidhaa mbalimbali ndani na nje ya maeneo yao.
  4. Wachungaji: hawa ndio waliokuwa wakijishughulisha na uchungaji wa wanyama na kazi ya kilimo kwa kiasi fulani.

Ama kwa upande wa kitabia,Waarabu za jahilia kama walivyo watu wa zama hizi walikuwa na tabia nzuri na nyingine mbaya. Miongoni mwa tabia njema walizokuwa nazo ni kama vile ukarimu, murua, ushujaa na utekelezaji wa ahadi. Tabia mbaya zilizoitawala jamii ile ni pamoja na ulevi, uchezaji wa kamari, ulaji riba na kuwazika watoto wa kike wakiwa hai kama ilivyoelezwa na Qur-ani:
"NA MTOTO MWANAMKE ALIYEZIKWA HALI YAKUWA YU HAI ATAKAPOULIZWA. KWA MAKOSA GANI ALIUAWA. (81:8-9)

 

SOMO LA TATU

i/NASABU YA MTUME KUUMENI KWAKE

Nasabu ya Bwana Mtume – Allah amrehemu na kumshushia amani – kwa upande wa baba yake ni kama ifuatavyo:-

Yeye ni Muhammad Bin Abdillah Bin Abdil – Mutwalib Bin Haashim Bin Abdi Manaf Bin Qusway Bin Kilaab Bin Murrah Bin Kaab Bin Luayyi Bin Ghaalib Bin Fihr Bin Maalik Bin Nadhr Bin Kinaanah Bin Khuzaymah Bin Mudrikata Bin Ilyaas Bin Mudhwar Bin Nizaar Bin Maad Bin Adnaan. Huu Adnaan ni katika kizazi cha Nabii Ismail Bin Ibrahim – Amani iwe juu yao.

ii/NASABU YA MTUME KUKENI KWAKE

Nasabu yake Bwana Mtume – Allah amrehemu na kumshushia amani – kwa upande wa mama yake:-

Yeye ni Muhammad Bin Aaminah Bint Wahab Bin Abdi Manaf Bin Zuhrah Bin Hakiym. Huyu Mzee Hakiym ndiye Kilaab ambaye ni babu wa tano wa Mtume kwa upande wa baba yake.

Tumekwishaeleza huko nyuma kwamba huyu Mzee Qusway ambaye ni babu wa nne katika mlolongo wa babu zake Mtume ndiye aliyeweka mpango wa mji wa Makkah na akawaunganisha pamoja Waarabu kwa kuondosha ukabila.

Baada ya kifo cha Mzee Qusway, hatamu za uongozi wa mji wa Makkah zilishikwa na babu wa pili wa Mtume Mzee Haashim. Huyu alikuwa tajiri na ndiye aliyeasisi mfumo wa biashara za Kusi na kaskazi kama ulivyoelezwa na Qur-ani:-
"ILI KUWAFANYA MAKURESHI WAENDELEE. WAENDELEE NA SAFARI ZAO ZA WAKATI WA KUSI (kwenda yaman) NA WAKATI WA KASKAZI (kwenda Shamu, ndio maana tukajaalia jeshi la ndovu kushindwa) (102:1-2)

Pia Mzee huyu ndiye aliyesimamia usambazaji wa maji na chakula kwa wageni wote wanaokuja kufanya ibada katika Al-kaaba na hili linaashiria ukarimu walikuwa nao Waarabu. Naye ndiye mtu wa mwanzo aliyeanzisha uokaji na usambaji wa mikate katika mji wa Makkah na hili linaonyesha ni jinsi gani alivyowajibika kwa jamii iliyompa dhamana ya uongozi.

Mwenyezi Mungu aliitakasa nasabu ya Mtume kutokana na uchafu wa kijahilia. Mababa zake wote walikuwa ni watu watukufu na viongozi kama ambavyo mamama zake pia walikuwa ni wanawake waungwana,watakasifu wasio na uchafu wowote.

Lifuatalo ni jedwali na kielelezo kinachoonyesha nasabu ya Mtume kuanzia kwa babu wake wa nne Mzee Qusway. Jedwali hili litatusaidia kuelewa koo za Maqureshi huko mbele.

 



Forum | Guestbook | Tuandikie |