|
Kuuawa Baniy Quraydhwah kwa kuchinjwa , kulikotokana
na amri ya Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie. Kuliacha athari
isiyofutika katika nafsi za Mayahudi, wakawa wametoshewa, wametunduwaa wasijue
la kufanya. Moto wa ghadhabu na uchungu ukitokota na kuwaka mioyoni mwao,
ukifunikwa na tabia ya unyonge na uoga iliyokita mioyoni mwao. Wakawa na hisia
kali za chuki na uadui zilizo changanyika na hisia kina za khofu na utisho.
Hapo hapo wakiwa na mapenzi makubwa ya kutaka kuangamiza na kuponya machungu
na ghadhabu yao. Mapenzi yao haya yakawa yanasukumwa na hisia za kusonga mbele
na kurudi nyuma na kuingia vitani kuliko kinzana na pupa ya kupenda mno uhai
kuliko kufa. Mayahudi walikuwa na udhuru katika muhemeo huu, kwani
walikwishapata kipigo kikali kisichosahaulika kutoka kwa Waislamu huko nyuma.
Na uzoefu umewaonyesha kwamba adui yao huyu ni mtu wa kuogopwa asiye wa
kawaida na mwenye nguvu nyingi. Na kwamba anapata msaada wa nguvu za haki
zisizoshindika na nguvu ya kibinadamu. Kwa hivyo basi, sio jambo rahisi kuweza
kushindana nae na ukafanikiwa kumshinda hata kama una nguvu kubwa kiasi gani.
Pamoja na kuyatambua na kuyakiri yote haya, bado Mayahudi walitamani kuzima
mioto yao ya moyoni. Kwa kulipa kisasi na kumuhilikisha adui yao huyu aliye
wadhalilisha na kuondosha haiba na heshima yao machoni mwa walimwengu.
Historia sahihi na ya kweli inaonyesha kwamba siku zota
Mayahudi ndio waliokuwa wachokozi wakianzisha shari. Na mara nyingi shari
waliyoianzisha wao iliwarudia wao wenyewe kwa kushindwa vibaya katika
mapambano waliyopata kuyawasha. Pamoja na kushindwa huku kwa mara kwa mara,
bado Mayahudi hawakukoma na kuacha uchokozi wao. Kama ambavyo hawakuwaidhika
wala kunasihika na matukio yaliyopita, wakauzingatia mustakbali wao kutokana
na yaliyopita.na wala kushindwa huko hakukuzituliza wala kuzifuta mioyoni mwao
hisia za chuki na uadui kuuelekea Uislamu na Mtume wake. Wakaweza kuishi na
Waislamu kwa amani na matangamano mema, hili halikupewa nafasi walau kidogo
nafsini mwao. Kinyume chake ni fikra moja tu ndio iliyozitawala akili na
mawazo yao, fikra waliyousiana viongozi na wakubwa wao. Hii haikuwa nyingine
zaidi ya kuutokomeza Uislamu na waislamu kadiri iwezekanavyo. Mara nyingine
fikra hii ikusukumwa na hisia za hasadi na wivu kwa nini utume umehama kwao na
kwenda kwa Waarabu. Wakati mwingine msukumo ulitokana na hisia za uadui na
chuki binafsi na pengine ni yale mapenzi yao ya kutaka kuangamiza na kulipa
kisasi. Kila walipoona wigo wa Uislamu unazidi kutanuka na kuimarika, ndio
fikra hii ovu ilipozidi kujikita mioyoni mwao. Wakiburuzwa chini ya taathira
zilizotokana na fikra hii, wakifikiri, wakipanga na kupangua namna ya
kuitekeleza. Wakitafuta na kuvizia sababu watakazozifanya mlango wa kupitia na
kuyafikia malengo yao.
II.
Uadui wa tangu kale
wakita mizizi nyoyoni:
Neno/kauli aliyoitamka kiongozi wao; Huyay Ibn
Akhtwa, tangu pale Mtume wa Allah-Rehema na Amani zimshukie-alipowasili
Madinah. Ikawa ndio desturi na kanuni waliyoshikamana na kuifuata Mayahudi
wote kuwaelekea waislamu, kwa maneno mengine ikawa ndio sera yao. Hii ndio
kauli yenyewe kama ilivyonukuliwa katika Rejea za Historia (tarekh): "Wallah
ni uadui tu maisha yote". Naam, ni kweli kauli hii ikawa ndio msingi
walioukumbatia Mayahudi wote tangu siku ilipotamkwa. Ikawa ndio sera
waliyoitumia viongozi na waongozwa wao na matukio yaliyojiri yakaendelea
kuichochea na kuiwasha mioto ya uadui huu. Na yakiudhihirisha katika mandhari
inayo onyesha wazi chuki yao dhidi ya mafanikio wayapatayo waislamu. Kwani
tangu pale waislamu walipopata ushindi dhidi ya mushrikina katika vita vya
Badri. Mayahudi wakaanza kudhihirisha dhahiri shahiri uchungu uliomo mioyoni
mwao kuelekea ushindi huu mnono wa waislamu. Mshairi wao mkubwa; Ka'ab Ibn
Al-Ashraf akatunga na kupita akiimba mashairi ya maombolezo akiwaombolezea
mushrikina waliouawa katika vita hivi. Na akiwahimiza na kuwachochea
Makureishi kulipa kisasi na wakati huo huo akitoa maneno machafu dhidi ya
wanawake wa Kiislamu. Kama alivyouachilia ulimi wake mchafu kuvinjari kinywani
mwake kumtukana na kumvunjia heshima Mtume na akila njama za kumuua pamoja na
Mayahudi.
Mshairi huyu mwenye ulimi mchafu alipopata jazaa yake sawia
kwa kuuawa na waislamu. Mayahudi wa Baniy Qayunqaa waliinuka na kuonyesha
upinzani dhidi ya waislamu na wakiwachochea kuingia vitani kwa kila kauli na
matendo yenye kuumiza hisia. Waislamu walipowafurusha kutoka Madinah, kazi yao
hii ikashikwa na Mayahudi wa Banin-Nadhwiyr ambao hawa walifanya jaribio
lililoshindwa la kumuua Mtume. Nao walipofukuzwa Madinah, kiongozi wao; Huyay
Ibn Akhtwab akaanza kukusanya makundi dhidi ya Mtume na waislamu. Na
akiwahimiza na kuwachochea Baniy Quraydhwah kuwasaliti waislamu katika
mazingira mabaya mno. Huyu nae alipopata ujira wa kazi yake hii chafu, nafasi
yake ikashikwa na Abu Raafii; Salaam Ibn Abil-Huqayq. Huyu akajipanga upya na
kuanza kukusanya majeshi shirika dhidi ya Mtume na maswahaba wake. Akiitumia
mali na utajiri wake aliokuwa nao pamoja na mamlaka//sauti yake kuyaunganisha
na kuyakusanya pamoja makabila kuwapiga vita waislamu. Huyu nae alipoulipia
uovu wake, nafasi na dhima yake ikachukuliwa na Useir Ibn Rizaam. Huyu tofauti
na watangulizi wake, akapanga mbinu zake mwenyewe zisizofuata nyayo za
wenzake. Yeye akafungua ushirika na matangamano na Baniy Ghatwfaan ili wawe
upande wa Mayahudi wakati Mayahudi wa Khaybar watakapoingia vitani na
waislamu.
|