Makala
Mwanzo
Uislamu-Utangulizi
Fiqhi na Sheria 
Akhlaaq-Tabia
Sira ya Mtume
Nasaha za dini
Maswali na Majibu
Uliza Suala la dini
Jiunge na Mtandao

 

  MASWALI NA MAJIBU-Masuala mengine ya Dini  


Masuala mengine ya Dini-Sehemu ya Tatu                              
 
  1. Je sheria inaruhusu muislam kuoa mke ambae ni askari katika mazingira tuliyonayo hapa tanzania ilhali inaeleweka kuwa katika mavazi tunayoyaona wakivaa wao na hata (manesi) huwa hayana hijabu na huku tunasisitizwa kuwa wanawake wa kislaam wajiendeleze kitaaluma ili waweze kufanyakazi kuinua vipato vyao ,sasa kama kazi zenyewe ndio hizo zinazozuia hijabu mnashauri vipi?
     Je ni nafasi ipi aliyonayo mwanamke katika kazi za uaskari kiislam ? kwani nimeangalia vita vya iraq nimeshangaa kuona kinamama wameshika silaha kuihami nchi yao je hawa walikuwa askri kabla ya vita ? na wanastahiki kuandaliwa kupigana vita kama wanaume? na kama ni hivyo sasa sheria inayosema mke ni pambo la nyumba katika uislam itakuwa na nafasi ipi?

  2. IKIWA MTOTO ANAFAHAMU YA KUWA MAREHEMU BABAAKE ALIKUWA NA BIASHARA KUBWA SANA LAKINI MSINGI WA ILE BIASHARA ALIPATA PESA ZILE ZA HARAMU. JE INAMJUZIA YULE MTOTO BAADA YA MZEE WAKE KUFA KURIDHI ILE MALI NA YEYE INGALI ANAJUWA ZILE PESA ZILIANZIA MSINGI WA HARAMU.

  3. naomba mnijibu  ili linalonitatiza.nini  maana  ya  mfungo?na  kwanini muharami  ambao  ni  mwezi  wa  kwanza  wa  uislamu ukaitwa  mfungo  nne, badala ya  kuitwa  mfungo  mosi?kwasababu  wenyewe ndio mwezi  wa kwanza.

  4. yale  maji  yanayomwaga  juu  ya  kaburi baada  ya  maiti  kufukiwa yana  maana  gani? ubao  unaofunikwa  katika  mwanandani  kaburini  una maana gani?

  5. Mimi ni muislam lakini kuna jambo moja linanitatiza sanaa!!! Kuhusu Kiarabu na Quran,ninavyojua mimi kuwa Quran ni lugha iliyoshushwa na mwenyezi mungu na sio ya watu furania au kabila fulani pia nafahamu kuwa maneno ya Kiarabu mengi yanafafana na Quran.Nabishana sana Na Wasio waislam wanavyosema wao wanajua kuwa Quran ni kiarabu na sisi tunafuata mila za kiarabu na kwahilo tumekuwa tukichukiwa sana na tunaambiwa sisi tuko nao pamoja na mimi nawajibu kuwa sisi na wao ni Dini moja kama nyinyi na wazungu wengi dunia kote. Kwahiyo basi naomba unipatie jibu sahihi ili nipambane na hawa wasiokuwa waislam.Nataka kukanusha kuwa quran si kiarabu maana kiarabu ni lugha ya watu na qurani lugha ya iliyoteremshwa na Mwenyezi Mungu

  6. je sheria ya dini ya kiislaam inasemaje kuhusu swala la kuangalia mtoto ndani ya tumbo kabla hajazaliwa kama ni wa kike au wa kiume?

  7. INAJUZU IKIWA UMEISHA CHAGUWA KITU UNACHO KITAKA DUKANI KWA SONARA, UMEWAFIKIANA NAYE UTAPELEKA PESA  KIDOGO KIDOGO MPAKA LILE DENI LAKE LIMALIZIKE NDIO ANIPE KITU CHANGU.

  8. kwaleo ningependa kuuliza suala linalo husu dada zetu na mama zetu pamoja na wakezetu imetokea kuwa kawaida kwa jinsia ya kike(wamejaaliwa) kupenda kujipamba sana na kupelekea kuzaliwa kwa mambo ambayo kabla hayakuwepo ili tu waonekane ni warembo. suala la kuweka dawa kwenye nywele lime kuwa ni kama kawaida kwa jamii ya leo na kila awekae dawa basi huwa na sababu zake

    kwa mfano mwingine huweka dawa ili:

    nywele ziwe laini

    nywele ziwe ndefu 
    sasa basi mafundisho ya dini yetu ya kiislam si jafahamu vizuri  imeliangalia suala hili kwa mytazamo gani 

  9. jee kumfananisha mkeo ni dhambi hata kwa yale mambo mengine?kwa mfano mtu kusema :mke wangu anafanana na ndugu yangu kwa nyusi zilivyo ungana,au mke wangu kama mama yangu kwa tabia yake fulaan {iliyonzuuri}"

  10. JE?KUNA HADITHI YEYOTE ILE INAYOHUSU MWANAMKE KUFUNIKA USO{NINJA}?NAKUHUSU KUVAA HIJAABU ILYOKUSUDIWA PALE NI SHUNGI AUJAPO MTANDIO ILHALI UMEFIKIA PALE ILIPOKUSUDIWA KISHERIA??


JIBU

 

Rudi Nyuma                                                  Endelea Mbele


| Tuandikie |