|
|
| |
MASWALI
NA MAJIBU-Ndoa na Talaka |
| |
|
| Ndoa
na Talaka-Sehemu
ya Kwanza |
|
|
|
|
|
- Naomba
kujua iwapo mwanamke aliye katika eda ya
kufiwa na mumewe, je wanaume ambao sheria inawaruhusu baada ya eda kumuoa
wanaruhusiwa kumuona kwa ajili ya kumpa pole
nina maana kuonana nao hata kama hawana nia
ya kumuoa,asante.
- naomba
kuuliza kuwa ni (a) haki ya mtoto wakike
kuchukuliwa mahari yake nawazazi wake kidini
ina uhalali, naomba jibu kwa ushahidi wa
qurani au hadithi ya mtume.
Ikiwa mtu halali na mumewe kwa muda mrefu na
anae ndani ya nyumba nini hukumu yake?
- je!mtoto
wa nje ya ndoa mtoto wa nje ya hali!na baba
mkristo na baba muislam atafuata dini ipi
katika hizo
- kama
tunavyojua kwamba ikiwa mwanamke anaachika
pindipo mumewe hawezi kazi ya kijamii (
kuingiliana) na mkewe, je! inafaa mwanaume
kufunga ndoa na mwanamke tasa (asiezaa kuzaa)?
au anaeumwa na maradhi ambayo hayamruhusu
kuzaa? naomba ufafanuzi
- suali
langu liko hapa! ikiwa kila mtu atachagua
mke mzuri na wakati sio wanawake wote wazuri,
Je! nani ataowa wale wabaya? je uchaguzi huu
wa wanawake ni halali?
- la
kwanza, Je kuna ruhusa yoyote ya kisheria
kwa mwanaume wa kiislam kutumia vijidonge
ambavyo havina madhara mwilini
ili aongeze nguvu za kiume? na hii inatoka
na malalamiko ya mkewe mtu kuwa bwana siku
hizi hunifikishi yaani unitoshelezi kama
zamani kulikoni? na magomvi haya yanapelekea
ndoa kuyumba kwa kila mmoja kuona kuwa
mwenzi ameshamchoka, je kuna ruhusa ya
kumuona mtaalam Dr ili aandike dawa
ambazo hazitokuwa na madhara ili amani
irudi kwenye nyumba hiyo?
swali la pili
nini hukumu ya kisheria ya mwanaume amabye
amekuwa akimtishia mkewe mara kwa mara
inapotokea kuto kuelewana mume hutishia
kuandika talaka nakuacha sasa hivi au toka
humu ndani, mwanamke amekuwa na heshima ya
uoga kwa mumewe kwa kutishiwa talaka, je
kuna uhalali wowote wa mume kumtishia
mara zote mkewe nakuacha huku ameshika
peni na karatasi?
- Nimefunga
ndoa ya kwanza na mke wangu ambayo ilikuwa
ya kimila kwa sababu mke wangu alikuwa
mkristo baadaye alibadilisha dini na kuamua
kufunga ndoa ya kiislamu siku mbili kabla ya
mfungo wa ramadhani.
Swali langu ni kwamba katika ndoa hiyo
hakuna hata wazazi waliofika katika ndoa
yetu kutoa baraka, si wazazi wa mke wangu
wala wazazi wangu? zaidi ya marafiki
zangu.Je swali langu nataka kufahamu je
kutofika kwa wazazi wa pande mbili katika
ndoa hiyo nitakuwa nimepata dhambi kwa
mwenyezi mungu
- Swali
langu la leo ni kuwa; Iwapo kuna mtu
aliyeowa kwenye mwaka 1950 kwabahati mbaya
hakumaliza mahali ina maana ana deni katika
hiyo mahari la shilingi 300/= na leo hii
mwaka 2003 anataka kulilipa; JE atalipa ile
ile shilingi 300/= au zaidi? asante.
- Mimi
kuna swala ambalo nigumu sana
linanitatanisha kuhusu KITOVU CHA
MTOTO-MCHANGA WA KIUME, kwamba eti kitovu
chake kitakapomdondikea katika uume wake
siku ya kukatika basi asilani uume wake
utakuwa haufanyi kazi-kabisa.
JE, NI KWELI?? na ikiwa ni kweli.
Naomba munijibu na ikiwa kama kuna ushahidi
katika Qurani au wa hadithi ya Mtume S.A.W,
au utafiti wowote uliyofanyika kuhusu swala
hili munifafanulie kwavyo. Nasisi waislamu
ni HARAMU kuitikadi mambo ambayo hayana
Dalili.
- mie mume wangu ni mlevi sana na miye na jitahidi sana kushika dini yangu,
nayeye pia namtoleya mawaidha ya deni
afahamu lakini bado anadharau na alokuwa ya
meharamishwa kwenye dini yeye anataka
niyafanye je huo mume ninfate tu maasi kama
hayo anasema nifanye kwani wanasema ibada
yako unafanya weye mwanamke haikubaliwi
mpaka mume wako ufatishe anayoyataka ufanye.
kwahisani yenu mnipe shauri yakufanya
JIBU
Endelea
Mbele
|
|
|
|
|
|
| |
|
|
| Tuandikie |
| |
|