|
|
|
|
|
| Swala-Sehemu
ya Kwanza |
|
|
|
|
|
- mimi
ni mkazi wa muda mrefu nje ya nchi yangu na
nitakuwa hapa kwa muda kiasi takriban miaka
mitano au zaidi kidogo, sasa je nini fatwa
ya mimi kuswali swala zangu kama msafiri? na
maanisha je kuna ruhusa ya mimi kuziswali
swala zangu kama msafiri kwa muda wote
nitakao kuwa hapa?
Na je ni vipi basi nitaziunganisha
kama kuna ruhusa hiyo? na je kama
inapatikana fulsa ya mimi kukamilisaha tano
kwa kujihisi upungufu fulani kwani kufanya
vile usivyozoea inakuwa taabu kwa siku za
mwanzoni , je inaruhusiwa baadhi ya
siku kuswali tano kwa wakati hata kama ni
utaratibu wangu kuzichanganya kama msafiri?
- IKIWA
MIMI NIMEZALIWA ZANZIBAR NA NIMEJENGA
ZANZIBAR LAKINI SIISHI NNAISHI OMAN, NA
NIMEJENGA NYUMBA OMAN NA NDIKO NNAKO ISHI JE
IKIWA NTAKWENDA ZANZIBAR KUTEMBEA NITASWALI
WATAN AU SAFAR?
- Mimi
nauliza kuhusu suala la isibali yaani
kuburuza suruali,je ni kweli kuwa yeyote
aswalie hali ya kuwa suruali au kanzu
inaburuzika swala yake ina mushkeli?Naomba
sana jibu liwe na ushahidi ili niweze
kuielimisha familia yangu
- naomba
kujuwa hukmu ya swala ya ijumaa.kwanza iko
kwenye kundi gani nifardhi ain kifaya ama
sunna.kisha hukmu ya mwenye kuacha ijumaa
bila ya sababu ni nini.
- Eti baada ya kusali swala yoyote ya
faradhi, kisha baada ya kutoa salamu
ni kharamu kumpa muislamu mwenzio mkono
kwasababu: (eti hii ilikuwa ni mila ya
wayahudi kunamtu wao alikuwa na kidole gumba
gutu cha mkono wa kulia kwahiyo wao walikuwa
wakifanya hivyo ili kuitikadi kwamba wapate
baraka kutoka kwake!)
Eti baada ya kusali si vyema kuomba dua
kwa pamoja kwasababu kila mtu anamatatizo
yake binafsi!.
- Huwa
napataga safari ya kutoka DSM kwenda TABORA
kwa usafiri wa TRENI kwa muda wa
mchana-mzima na usiku-mzima hadi saa 4:00
usiku ndio nafika nyumbani
(i.)Ndani ya treni hakuna maji ili nichukuwe
udhu (Je, nifanyeje?).
(ii.)Vile vile pakusalia hakuna, hata kama
nikiamua kusali kwa ishara (ikiwa udhu
nitakuwa nao) kutokana na ghasia, msongamano,
mara mtu anakuomba kwamba simama kidogo ili
nichue au niweke kitufulani chini ya kiti;
na Mfano wa kama hayo. (Je, nitasali vipi?)
(iii.)Na hili swala la kwamba ukiwa safarini
waweza kupunguza SALA zenye rakaa 4 ukasali
2, na waweza kusali kwa pamoja Adhuhuri na
Alasiri kutokana na ile misukosuko ya
ugenini (Je, jambo hili nikweli kwa ushahidi?)
(iv.)Na katika Swala la kutengukwa na udhu
kuna kipengere cha kwamba "Ukigusana
ngozi kwa ngozi na mwanamke unaeweza kumuoa
kisheria udhu wako unatenguka" Sasa je,
kwa hali hii utafanyaje ikiwa unao udhu
kisha ukapanda kipando au basi-tauni
ukielekea msikiti wa ijumaa halafu ikatokea
kugusana na mwanamke, na baada ya kufika
huko maji hakuna.?
(v.)Kwa mtu aliyeko mahabusu (Je, Ata Sali
vipi na ni mahala pachafu?, Atapata wapi
udhu?
- je,nikiswali
nyuma ya imamu mshirikina(yaani mpiga
ramli)swala yangu itasihi?
pili: je,nikiingia
msikitini kusali sala ya ijumaa hali ya kuwa
nimechelewa rakaa zote mbili lakini
nimemkuta imam kwenye tahiyatu,je nitanuia
kuswali jumaa au dhuhuri?
mwisho: naomba
ufafanuzu juu ya sala yenye tahiatu
nne.(yaani mfano mtu kamuwahi imam kwenye
tahiatu ya kwanza kwenye sala ya magharibi
akaa kisha tahiatu ya mwisho kwa imam nae
akakaa kisha imam alipotoa salamu kwake
ikawa ndio kwanza kamaliza rakaa moja hivyo
baada ya kunyanyuka akasali rakaa ya pili
akakaa tahiatu kisha akanyanyuka na kumaliza
rakaa ya mwisho akakaa tahiatu ya mwisho)
kama nimeeleweka vizuri itakuwa huyu mtu
kakaa tahiatu nne.je sala hii haitakuwa na
dosari yoyote?
- Mtume
wetu ametusisitiza sana juu ya kusali
msikitini kwa wanaume.
je mwanaume anaruhusiwa kusali nyumbani
ikiwa anaogopa akitoka kwenda msikitini
pengine waizi watavunja nyumba yake na
kuiba?au pengine ni sala ya asubuhi nae
anaogopa pengine atavamiwa na majambazi au
labda anaweza kuumwa na mbwa?
- Katika
kufunga mikono katika sala naona kila mmoja
anafunga vyake
atakavyo,yaani kuna wanaofunga chini ya
tumbo,kuna wanafunga tumb
oni,na pia kuna wanaofunga chini
yamaziwa,pia kuna wafunga juu ya
kifua,na kuna wanio achia kabisa
hawafungi,mimi nataka ufafanuzi
kuhusu jambo hili,yaani ipi iliokuwa SAHIHI.
- 1)Iwapo
nitakuwa kazini mchana hadi jioni na swala
ya Alaasir ikanipita nikifika ni magharib
jee nitaswali magharib ndio nilipe ya alasir
au nitaswali Magharib kwanza kwani ndio muda
au muadhini wa magharib ameshaadhini?Naomba
ufafanuzi wako!
2)Jee Inawezekana wakati naswali adhuhuri
nikaswali swala ya alasiri kama swala ya
safari!Kwa sababu muda wote wa alasir
ninakuwa kazini na hakuna mahala ambapo
naweza kujihifadhi nikaswali swala hiyo ya
alasir1
JIBU
Endelea
Mbele
|
|
|
|
|
|
| |
|
|
| Tuandikie |
| |
|