- swali
langu ni juu ya hili swala la mwezi hakika
kuna mpingano kati ya makundi ya kiislamu
kila kundi linatoa dalili zake hii
inakuwaje?na wakati wote tunahukumu kwa
kitabu kimoja QURAN na sunna za
mtume(s.a.w)naomba maelezo kwa dalili lipi
ni sahihi katika tofauti hizi
- Mimi
nikijana niliyeowa ninafanyakazi ya
ulinzi,wakati wa mwezi mtukufu wa ramadhan
nimepangiwa kuanza kazi saa 11.30pm kabla ya
salaatul maghrib na ninatoka kazini 12.00am
baada ya salatul fajr,ni kipindi cha mchana
tu ambacho ninachoweza kuwa na mke wangu jee
pindipo ninaposhikwa na hamu ya mke kufanya
nae mapenzi jee nihalali na kama ni haramu
mimi nishafanya nae mchana jee ni hukumu
gani nitaipata kwa dini yetu, na jee ikiwa
yeye ameshikwa na hamu hiyo nimfanye nini.
- mimi
nauliza jee,ikiwa hukufunga ramadhani ya
mwaka juzi natakiwa vipi au
unatakiwa ulipe fidia .Hiyo ramadhani
nilikuwa ni mjamzito na sikuweza kufunga kwa
kunyonyesha .
- mimi
nipo Malaysia sasa, na nataka kurudi
nyumbani Unguja wiki ijayo ambayo itakuwa ni
Ramadhani. Suala langu ni kuwa safari yote
kutoka hapa hadi Unguja ni karibu masaa 24
kwa ndege, jee napaswa kufunga? mimi nafsi
yangu naona kama nitajikalifsha. Naomba
ufafanuzi. Ahsante
- Mimi
na wasi wasi juu ya kutumia dawa ya meno
wakati umefunga, jee inakubaliwa kutumia
dawa au haikubaliwi. Naomba jawabu la
kunitoa wasi wasi huu.
- Tafadhali
sheikh, nimesikia kutoka kwa masheikh kwamba
kufunga siku ya IDD EL-fitri ni dhambi kubwa
kwani siku hii ni sikukuu. sasa nauliza
kwamba je itakuwaje ikiwa mtu hufahamu yupi
sahihi kati ya wale wanaofungua siku moja
kabla ya mwezi kuandama[Ansar Sunn] na
BAKWATA? na je itakuwaje ikiwa BAKWATA wapo
sahihi na mimi nimewafuata Ansar Sunn
kusheherekea IDD EL-Fitri wakati kumbe mwezi
bado haujaandama? je ni dhambi kubwa?
- Kuna
mtu ambae yuko nchi za ng'ambo ambazo si ya
kiislamu, kazi yake ni kumpikia bosi wake
pamoja na wageni wake,sasa katika kipindi
hichi cha Ramadhan inamlazimu mtu huyo
kuendelea na huduma zake hizo ilhali yeye
yumo kwenye funga. Sasa je funga yake
inakubaliwa mtu huyo, ukizingatia kuwa
pindipo ataacha kufanya hiyo kazi au
kuchukuwa likizo basi kurejea kazini itakuwa
ni vigumu na kutafuta kazi nyingine vile
vile ni vigumu sana na yeye yuko ugenini
hana jamaa wa kumtegemea? Naomba jawabu yako
unipe na ushahidi.
8.
mimi
ninafunga ila nina matatizo ya tumbo vidonda vya
tumbo. huwa ninajitaidi kufunga siku tatu au nne
na ya tano huwa ninapumzika navuta nguvu je
swaumu yangu itakubalika .
- nilikuwa
nauliza je wanawake pia ni lazima wasali
taraweh?
- Swali langu lahusu swaum.Mimi nadaiwa siku 15 za swaum,swali je naweza
kuzilipa katika mwezi huu wa shabaan au
haiswihi?
Je kama haiswihi naweza kuzilipa baada ya
swaum ya mwaka huu?
JIBU
Endelea
Mbele
|